Powered By Blogger

Monday, May 30, 2011

Mama akamatwa na polisi kwa kuuza bikira ya Mwanae: Tsh 15 Millioni

Mama mmoja kwa jina la Felicia Rea Mclure miaka 32 anayetoka katika mji wa  Salt Lake nchini Marekani, amefunguliwa mashtaka kwa kosa la kutaka kuuza Bikira ya mwanae mwenye umri wa miaka 13 kwa Dola 10,000 za Marekanai sawa na zaidi ya Tsh million 15  za kitanzania.

Bikra ya binti huyo ilikua iuzwe kwa bwana mmoja aliyejulikana kwa jina la Don. Binti huyo aliieleza Mahakama kwamba awali alikubali kufanya ngono na Don kulingana na makubaliano yaliyofikiwa baina yake, Don na mama yake; lakini baadae aliamua kukataa.

Mwanamama Felicia Re McClaure

Mpango wa mama huyo ulitibuka baada ya rafiki wa kiume"boyfriend" kukuta mlolongo wa ujumbe wa simu za mkononi ikielezea namna ambavyo mama huyo alipanga kutekeleza udhalimu huo. Mama huyo alikiri kwamba aliwahi kumpeleka Binti yake kwa Don ili kumuonesha namna alivyoumbika.

Mama huyo vilevile anakabiliwa na kosa la kumpiga picha za utupu binti yake huyo na kwenda kuziuza kwa wanaume na hatimaye kujipatia fedha.Hakimu ya mahakama hiyo ya Wilaya amebainisha ya kwamba, uchunguzi bado unaendelea ili kumpata Don na wanaume wengine ambao waliwahi kuuziwa picha na mwanamama huyo.
Mahakama ya Wilaya ya Utah

Felicia ambaye amekiri kutenda makosa hayo , anakabiliwa na mashtaka mawili katika Mahakama ya Wilaya ya Utah, mosi ni kosa la unyanyasaji wa ngono na mengine mawili ya unyonyaji wa kingono kwa mtoto mdogo. Mama Huyo kwa sasa yuko rumande baada ya kukosa dhamana ya Dola 250,000 sawa na zaidi ya shilingi Millioni 380 za kitanzania. Iwapo mwanamama huyo atapatikana na hatia atahukumiwa kusota jela kwa miaka mingi.


Friday, May 27, 2011

Takukuru yagonga mwamba kwa Mwakalebela na mkewe.

Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru), imegonga mwamba kwa mara ya pili, baada ya Mahakama ya Hakimu Mkazi Mkoa wa Iringa, kutupilia mbali kesi ya kutoa rushwa katika mchakato wa kura za maoni ndani yaCCM, iliyokuwa ikimkabili kada wa chama hicho, Frederick Mwakalebela na mkewe Selina.

Mwakalebela alikuwa mshindi wa kwanza katika kura za maoni zilizoendeshwa na CCM Manispaa ya Iringa, mwezi Agosti mwaka jana, lakini vikao vya juu vya chama hicho viliondoa jina lake kwa tuhuma za kutumia rushwa.

Katika kesi hiyo, Mwakalebela na mkewe Selina, kwa pamoja walikuwa wakituhumiwa kutoa hongo ya Sh. 100,000 kinyume cha sheria namba 15 (1) , (b) ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa, ambayo inasomwa kwa pamoja na kifungu cha 21 (1) , ( a) na 24 (8) ya Sheria ya Gharama za Uchaguzi ya mwaka 2010.

Akisoma uamuzi mdogo wa mahakama kuhusu pingamizi lililo wasilishwa mahakamani hapo na Takukuru, Hakimu Mkazi Mkoa wa Iringa, Mary Senapee, alisema baada ya kupitia kwa kina pingamizi lililowekwa na upande wa utetezi na kusikiliza maelezo ya upande wa mashataka, ameridhika na hoja zilizotolewa na upande wa utetezi na hivyo haoni haja ya kuendelea na shauri hilo.

Mwakalebela akiwa Mahakamani
Hakimu Senapee alitupilia mbali shtaka hilo huku akitoa uhuru kwa Takukuru kukata rufaa Mahakama Kuu kama hawajaridhika na uamuzi wa mahakama hiyo.Takukuru iliwakamata kwa mara ya pili washitakiwa hao mwezi Machi mwaka huu, na kuwafungulia upya mashataka chini ya hakimu mwingine, baada ya kurekebisha kasoro zilizojitokeza katika shtaka la awali ambapo ilibainika kuwa walifunguliwa shitaka moja kwa kutumia sheria mbili tofautiHata hivyo, kitendo cha kulirejesha tena mahakamani hapo shtaka hilo kuliwekewa pingamizi la kisheria na upande wa utetezi kupitia wakili wa Mwakalebela na Mkewe, Basil Mkwata ambaye amesisitiza kuwa Takukuru walifungua shitaka jingine kwa makosa yale yale na kusema kuwa sheria ya gharama za uchaguzi ya mwaka 2010 inasisitiza makatazo ya kimaadili na hivyo makatazo sio makosa ya jinai kisheria. CHANZO: NIPASHE

Thursday, May 26, 2011

Wauhumiwa wa EPA wawasilisha rufani yao.

Rajabu Maranda na binamu yake, Farijala Hussein waliohukumiwa kutumikia kifungo cha miaka mitano jela baada ya kupatikana na hatia ya kujipatia kwa njia isiyo halali Sh1.8 bilioni, kutoka katika  Akaunti ya Madeni ya Nje (Epa) katika Benki Kuu ya Tanzania, wamewasilisha rufani kupinga hukumu hiyo.

Rufani hiyo iliwasilishwa jana na wakili wa utetezi Majura Magafu, katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, kwa kile alichodai kuwa wateja wake hawakurishwa na hukumu hiyo.Alisema kwa sababu hiyo, wameamua kukata rufani katika Mahakama Kuu ya Tanzania, ili ikibidi itengue hukumu hiyo na wateja wake waachiwe huru.

Hukumu dhidi ya warufani hao ilitolewa Jumatatu iliyopita na Hakimu Mfawidhi wa Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, Ilvin Mgeta, ambaye alifanya hivyo kwa niaba ya jopo la mahakimu watatu.
Mahakimu wengine waliosikiliza kesi hiyo iliyovuta hisia za watu wengi ni Focus Bampikya na Saul Kinemela.

Katika hukumu hiyo, hakimu huyo alisema mahakama ililiridhika kuwa washtakiwa walitenda kosa hilo. Washtakiwa katika kesi hiyo walikuwa wanakabiliwa na mashtaka manane ambayo ni kula njama, kughushi, wizi, kuwasilisha hati za uongo na kujipatia fedha kwa njia ya udanyifu.

Ilidaiwa kuwa washtakiwa walijipatia  Sh 1.8 bilioni kutoka katika akaunti ya Epa baada ya kuonyesha kuwa kampuni yao ya Kiloloma & Brothers imepewa idhini ya kukusanya deni la Kampuni ya BC Cars Export ya Mumbai, India.Katika  hukumu hiyo, iliamuriwa kuwa baada ya kifungo, washtakiwa watalazimika kurejesha Sh 1.8 bilioni  walizochukua na kwamba vinginevyo, watafilisiwa mali zao.

Wednesday, May 25, 2011

Wastaafu Afrika ya Mashariki: Washindwa Kesi.





Baadhi ya wastaafu wa Afrika ya Mashariki
WASTAAFU wa iliyokuwa Jumuiya ya Afrika Mashariki, jana walizua tafrani katika viwanja vya Mahakama Kuu ya Tanzania, kufuatia kitendo chao cha kufunga Barabara ya Kivukoni kwa zaidi ya saa nne.Tafrani hiyo ilisababisha kufungwa kwa lango kuu la kuingilia katika jengo la mahakama kuu, baada ya wastaafu hao kutaka kuingia ndani ya jengo hilo hukuwa wakiwa wamejawa na jazba.

 wastaafu hao walizua tafrani hio kutokana na kesi yao  ya madai ya Shilingi 2 Trilioni dhidi ya serikali kutupiliwa mbali na mahakama kuu.Hukumu iyo iliyosomwa kwa lugha ya kiingereza na kuchukua muda wa saa zima, ilitupilia mbali madai ya walalamikaji hao na kupelekea tafrani hio baada ya wafanyakazi kutokuridhika Chombo hicho cha kutoa haki.

Jitihada za Charles Semgalawe  wakili anayewatetea ndugu, jamaa na baadhi ya wasataafu wa jumuiya hio kuwaomba kuondoka katika maeneo ya mahakama ziligonga mwamba kwani  baada ya kuwaambia suala la kuondoka baadhi ya wastaafu walianza kufunga barabara ya kivukoni kwa kuweka mawe yaliyokua karibu na mahakama na wengine waliamua kulala barabarani. Hata hivyo Tafrani hio ilizimwa na polisi mnamo mida ya saa tisa alasiri baada ya kuondoa vizuizi vya mawe vilivyowekwa na awastaafu hao, na kutoa nafasi ya magari mengine kupita.

Kwa mujibu  wa Mwenendo wa sheria za madai, wastaafu hao bado wana nafasi ya kupinga hukumu hiyo katika Mahakama ya Rufani ya Tanzania.