Powered By Blogger

Monday, September 17, 2012

Majaji kesi ya Lulu 'wawazodoa' mawakili pande zote


Mojawapo wa Picha za Lulu akiwa Mahakamani
Gazeti la Majira limeandika; MAWAKILI wa pande zote mbili katika shauri la umri wa mshtakiwa wa kesi ya mauaji ya Elizabert Michael 'Lulu' wamejikuta katika wakati mgumu wakati wa uwasilishwaji wa hoja za shauri hilo katika Mahakama ya Rufaa.

Mawakili hao walikutwa na hali hiyo mahakamani hapo jana baada ya Jopo la Majaji watatu wanaosikiliza shauri hilo kuwahoji kuwa wanabishania umri wa mshtakiwa huyo ili iweje?, ikiwa kesi ya mauaji husikiliwa katika Mahakama Kuu hata kama kosa hilo likiwa limetendwa na mtoto mwenye umri wa mwaka mmoja.

Jopo la majaji wanaosikiliza shauri hilo ni Jaji Benard Luanda, Jaji January Msoffe na Jaji Benard Mtakagwa.

Jaji Msoffe aliieleza mahakama hiyo kuwa suala la umri lingeweza kutazamwa katika utolewaji wa hukumu hata kama wasingeomba mshtakiwa huyo achunguzwe umri wake.

Alisema  suala hilo pia  lingeweza kuingizwa wakati kesi hiyo itakapofikishwa Mahakama kuu wakati wa uwasilishwaji wa hoja za awali.

Alisema  malumbano hayo hayamsaidii mshtakiwa huyo kwani anaendelea kusota lumande kwa sababu katika kesi za mauaji sheria ya mtoto haihusiki.

"Kesi itahamishiwa Mahakama Kuu hata Kama inamuhusu mtoto wa miaka saba,ubishani wa umri kuanzia Mahakama ya Kisutu hadi hapa ili iwe nini?"alihoji Jaji Msoffe

Naye Jaji Luanda alihoji mawakili hao kuwa wanalumbana umri ili iwe nini, kwani kosa la mauaji hata kama likimhusisha mtoto wa umri wa mwaka mmoja sheria ya mtoto haihusiki.

Alisema  labda upande wa utetezi uieleze  mahakama hiyo kuwa mtoto wa miaka 17 hashtakiwi kwasababu mshtakiwa huyo sio wa kwanza kushtakiwa kwa kesi ya mauaji.

Wakati akiwasilisha hoja za upande wa mashtaka,wakili wa serikali mwandamizi Faraja  Nchimbi alidai kuwa msingi wa malalamiko yao ni dosari zilizojitokeza katika uamuzi uliotolewa na Mahakama Kuu na Jaji Fauz Twaib.

Alidai  uwauzi wa Mahakama hiyo kukubali kufanya uchunguzi wa umri wa mshtakiwa huyo haukuwa sahihi kwa sababu katika uamuzi wake Jaji Dkt.Twaib alikiri kuwa maombi ya upande wa utetezi hayakuwasilishwa mahakamani hapo kihalali kwa mujibu wa sheria.

Alidai kuwa,hivyo jaji huyo hakupaswa kukubali kuendelea kufanya uchunguzi na badala yake angetupilia mbali ombi hilo.
Alidai kuwa  Jaji huyo alikosea kutoa tafsiri ya kifungu namba 44(1) cha sheria ya Mahakimu na kwamba alipaswa kutoa maelekezo kwa Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu katika uamuzi wake.

Aliongeza kuwa waliomba mahakama ya rufaa ifanye marejeo ya uamuzi wa Jaji Twaibu badala ya kukata rufaa kwakuwa marejeo husikilizwa haraka ukilinganisha na rufaa.

Kwa upande wake wakili wa utetezi Bw.Peter Kibatala akiwasilisha hoja zake alidai kuwa hoja yao ya msingi kutaka umri wa mshtakiwa huyo uchunguzwe ilikuwa kulida maslahi ya mtoto.

Kibatala alidai kuwa kulinda maslahi hayo sio tu shauri hilo kuhamishiwa mahakama ya watoto bali pia  katika utolewaji wa adhabu hukumu itakapofika.

Alidai kuwa hawakuwa na namna ya kuingiza ushahidi wa umri wa mshtakiwa huyo isipokuwa kwa njia hiyo.

Kibatala alisema  msimamo wa upande wa utetezi ni kwamba shauri hilo lirudishwe katika Mahakama ya Kisutu liendelee na taratibu za awali za kimahakama.

Katika kesi hiyo Lulu anakabiliwa na kesi ya mauaji katika Mahakamaya Hakimu Mkazi Kisutu,ambapo anadaiwa kumuua msanii mwenzake, Steven Kanumba Aprili 7, mwaka huu. Chanzo gazeti la Majira.

Thursday, September 13, 2012

Juror says he’s too homophobic and racist to serve, now faces prosecution.

A British man who said his "extreme homophobic and racist views" should make him ineligible for jury duty now faces prosecution over the claim.The Daily Echo reports that the man's identity is being kept anonymous for now but that Judge Gary Burrell QC read the leader in open court. In the letter, the man writes:
"I strongly believe that it would be a serious injustice to the legal system to select me for jury service.

"I hold extreme prejudices against homosexuals and black/foreign people and couldn't possibly be impartial if either appeared in court. Therefore it would not be in the court's interest to have me a juror."

In addition, the man said that if he were selected, he also would not pay attention to the case and would simply vote with the majority.The man had been selected to serve on a jury in the case of a man on trial for assault and reckless driving. And while Burrell questioned the authenticity of the man's claim, he nonetheless dismissed him from jury duty.

Though he escaped jury duty, the man could soon find himself on trial. The prosecutor and defense attorneys in the case, barristers Rebecca Austin and Robert Bryan, stepped outside their traditional role of legal combatants to lodge a joint complaint against the man.
  
Under Britain's Contempt of Courts Act, he could face prison time or a fine for failing to serve on jury duty

"The Attorney General's Office is aware of this case, and we await more information from Judge Burrell," said a spokesman for the Attorney General's Office.

Wednesday, September 12, 2012

TUHUMA KWA MAJAJI"MDAU" AMJIBU TUNDU LISSU


Katika pita pita zangu katika mitandao ya kijamii, hususani katika mtandao marufu wa” Jamii Forums” nimekutana na majibu ya mdau juu ya hoja inayotikiza muhimili wa Makama nchini iliyoibushwa na Mh. Tundu Lissu katika kuchangia bajeti ya Wizara ya Katiba na Sheria Mwezi uliopita. 

Kimsingi Mh. Tundu lissu aliwasilisha utetezi wake kwenye kamati ya maadili ya bunge baada ya kutakiwa  kufanya hivyo na uongozi wa bunge. Yumkini, wiki iliyopita Mh. Tundu Lissu katika kikao cha Mawakili( TLS) kilichofanyika katika ukumbi wa AICC, name nikipata fursa ya kuudhulia aliendelea kuanika wazi mambo mbalimbali yanayo husiana na Muhimili wa Mahakama hususani Majaji.

Hivyo  basi nineona nibora nikuletee alichaoandika Mdau huyo wa Jamii Forums kama ifuatavyo:

Nimeshangazwa sana na hatua ya Mh. LISSU ya kuvunja Kanuni za Bunge na kutawanya katika magazeti kile alichokiita utetezi wake bila kujali haki asilia ya wale anaowatuhumu. Nitashangaa kama Bunge litashindwa kulinda hadhi na heshima yake kwa kutomchukulia Mbunge huyu hatua kali za kinidhamu.

Nimeshangazwa sana pia na hatua ya MH. LISSU kuendelea kulalamika katika Mkutano wa Mawakili na kutaka MAJAJI ALIOWATUHUMU WAONDOLEWE bila ya yeye kuchukua hatua za KIKATIBA.

Mh. LISSU na “WANASHERIA-HARAKATI” wenzako, nchi yetu iaongozwa na sheria na sio na kulalama.

Ni Katiba hii hii ya Jamhuri ya Muungano ambayo imempa Mh. Lissu Ubunge, vinginevyo ni watu wachache sana walikuwa wanamfahamu Tundu Lissu kabla ya kuukwa UBUNGE. Na ni kwa kutumia KINGA YA Katiba hii hii ambayo ndiyo Mh. Lissu anaitumia kuwatuhumu na kuwahukumu MAJAJI na Mhimili wote wa MAHAKAMA.

KINGA YA KIKATIBA YA UHURU WA KUONGEA ANAYOTUMIA MH. LISSU

Ni katiba hiyo hiyo iliyompa uhuru wa kuongea Mh. Lissu, ndio hiyo hiyo iliyowapa majaji kinga na kuondolewa kwa utaratibu maalumu. Kinga anayotumia Mh. Lissu kuwatukuhumu na kuwahukumu Majaji ni IBARA ya 100 inayosema:

100. Uhuru wa majadiliano na utaratibu wa shughuli bungeni
(1) Kutakuwa na uhuru wa mawazo, majadiliano na utaratibu katika Bunge, na uhuru huo hautavunjwa wala kuhojiwa na chombo chochote katika Jamhuri ya Muungano, au katika mahakama au mahali penginepo nje ya Bunge.

(2) Bila ya kuathiri Katiba hii au masharti ya sheria nyingine yoyote inayohusika, Mbunge yeyote hatashtakiwa au kufunguliwa shauri la madai mahakamani kutokana na jambo lolote alilolisema au kulifanyw ndani ya Bunge au alilolileta Bungeni kwa njia ya maombi, muswada, hoja au vinginevyo.


Pamoja na Wabunge kuwa na Kinga, Katiba hiyo hiyo iliyowapa waheshimiwa Wabunge KINGA pia inampa Mh. Rais KINGA, na pia inawapa Majaji KINGA na utaratibu wa kuwaondoa majaji kwenye nafasi zao za ujaji. Ibara zinazotoa kinga kwa Mahakama ni hizi. Ibara ya 107B IMETAMKA KUWA KATIKA KUTEKELEZA MAMLAKA YA UTOAJI HAKI, MAHAKAMA ZOTE ZITAKUWA HURU NA ZITALAZIMIKA KUZINGATIA TU MASHARTI YA KATIBA NA YALE YA SHERIA ZA NCHI.

UTARATIBU WA KATIBA KUWAONDOA MAJAJI WENYE TUHUMA
 Kama ilivyo kuwa kuna utaratibu wa KIKATIBA NA KISHERIA kwa Mbunge kupoteza Ubunge, pia zipo taratibu za KIKATIBA Rais kuondolewa kutoka ofisi ya Rais na MAJAJI kuondolewa kutoka katika nafasi zao za UJAJI. Tanzania ni nchi ya utawala wa Katiba, Sheria na taratibu!

Ni matumaini yangu kuwa Mh. LISSU aliapa kuilinda na kuitetea Katiba na sheria za Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Kwa kuwa Katiba ya Tanzania imetoa utaratibu wa kupokea tuhuma dhidi ya Majaji na Mahakimu na namna ya kushughulikia tuhuma hizo. Nitaeleza baadaye kwa nini mimi nadhani Mh. Lissu anatumia isivyo KINGA yake ya Ubunge kwa kulalamika KISIASA bila kuchukua hatua za KIKATIBA NA KISHERIA.

Mh. Lissu anaweza kutoa hoja kuwa haipendi KATIBA ya sasa. Lakini hii ndio KATIBA iliyompa ngazi ya kupanda na kuwa Mh. Mbunge. Hii ndio Katiba iliyo halali inayofanya watanzania wamsikilize Mh. Lissu hata kama wengine hawakubaliani naye!! Tanzania nchi pekee ambayo utakuta Mbunge akilaani na kulaumu mfumo wa Katiba na sheria alioutumia kuupata ubunge.

Kama Mh. Lissu haipendi KATIBA YA JAMHURI YA MUUNGANO, basi aachie kiapo chake cha Ubunge na ajiuzulu UBUNGE ili afanye uharakati wa kupata Katiba anayopenda. Sio uungwana na sio sheria kutumia Katiba kupata daraja la Ubunge na mara baada ya kupata Ubunge kuihujumu Katiba hiyo hiyo.

KUWAONDOA MAJAJI KUTOKANA NA MARADHI, TABIA MBAYA Kwa mujibu wa Katiba, kuna utaratibu wa kikatiba wa kumtuhumu na kuondolewa kwa JAJI.

 JAJI ANAWEZA KUONDOLEWA
kama itathibitishwa na Tume MAALUM kuwa ameshindwa kutekeleza kazi zake (ama kutokana na maradhi au sababu nyingine yoyote) au kwa sababu ya tabia mbaya inayoathiri Maadili ya Kazi ya Jaji au Sheria ya Maadili ya Viongozi wa Umma.

Kamwe JAJI haondolewi kwa mayowe, kelele au vigelegele vya kisiasa. Jaji haondolewi kwa umahiri wa uongeaji wa Mh. Mbunge. Tusiwadanganye watanzania kuwa Mbunge Lissu anao uwezo wa kumuondoa JAJI yoyote kwa yeye kumtuhumu, kumtia hatiani na kumtaka aondoke bila kufuata utaratibu wa Kikatiba.

Mh. Lissu, kama unavyotegemea kinga ya Wabunge kwa mujibu wa Ibara ya 100 ya katiba, kumbuka kuwa Majaji, Rais pia wanayo kinga ambayo wewe pia ni vyema uiheshimu.

Mh. Lissu, IBARA 110 inazungumzia namna ya kumuondoa JAJI. JAJI haondolewi kwa kuwa tu Mbunge (Mh. Lissu) katoa tuhuma na kuchukua jukumu la kuithibitisha yeye mwenyewe na kudai JAJI aliyemtuhumu aondolewe. Huu ni utaratibu mpya sana ambao Mh. Lissu anautangazia umma wa Tanzania.

 IBARA ya 110 inayoratibu namna ya kumuondoa JAJI inatamka:
110-(5) Jaji wa Mahakama Kuu aweza tu kuondolewa katika madaraka ya kazi ya Jaji kwa sababu ya kushindwa kutekeleza kazi zake (ama kutokana na maradhi au sababu nyingine yoyote) au kwa sababu ya tabia mbaya inayoathiri Maadili ya Kazi ya Jaji au Sheria ya Maadili ya Viongozi wa Umma; na hataweza kuondolewa kazini ila kwa mujibu wa masharti ya ibara ndogo ya (7) ya ibara hii.

(6) Iwapo Rais anaona kuwa suala la kumwondoa Jaji kazini lahitaji kuchunguzwa, basi katika hali hiyo mambo yatakuwa ifuatavyo–

(a) Rais atateua Tume ambayo itakuwa na Mwenyekiti na Wajumbe wengine wasiopungua wawili. Na huyo Mwenyekiti na angalau nusu ya Wajumbe wengine wa Tume hiyo itabidi wawe watu ambao ni Majaji wa Mahakama Kuu au Mahakama ya Rufani katika nchi yoyote iliyomo kwenye Jumuiya ya Madola;

(b) Tume hiyo itachunguza shauri lote halafu itatoa taarifa kwa Rais kuhusu maelezo ya shauri hilo lote na itamshauri Rais kama huyo Jaji anayehusika aondolewe kazini kwa mujibu wa masharti ya ibara hii kwa sababu ya kushindwa kufanya kazi kutokana na maradhi na sababu nyingine yoyote au kwa sababu ya tabia mbaya.

(7) Ikiwa Tume iliyoteuliwa kwa mujibu wa masharti ya ibara ndogo ya (6) itamshauri Rais kwamba Jaji ambaye habari zake zimechunguzwa na hiyo Tume aondolewe kazini kwa sababu ya kushindwa kufanya kazi kutokana na maradhi au sababu nyingine yoyote au kwa sababu ya tabia mbaya, basi Rais atamwondoa kazini Jaji huyo anayehusika.

(8) Ikiwa suala la kumwondoa Jaji kazini limepelekwa kwenye Tume kwa ajili ya uchunguzi kwa mujibu wa masharti ya ibara ndogo ya (6) ya ibara hii, Rais aweza kumsimamisha kazi Jaji huyo anayehusika, na Rais aweza wakati wowote kufuta uamuzi huo wa kumsimamisha kazi Jaji huyo, na kwa hali yoyote uamuzi huo utabatilika ikiwa Tume itamshauri Rais kwamba Jaji huyo asiondolewe kazini.

(9) Masharti ya ibara hii yatatumika bila ya kuathiri masharti ya ibara ndogo ya (12) ya ibara ya 109 ya Katiba hii.
Utaratibu wa kumuondoa Jaji kwa mujibu wa Ibara ya 110 ya Katiba unazingatia msingi muhimu wa katiba ambao Mh. Lissu amewanyima Majaji aliowatuhumu, yaani haki ya kusikilizwa kabla ya kuhukumiwa kwa mujibu wa Ibara ya 13 (6) (a) na (b) ya Katiba yaani:-
- haki ya MAJAJI waliotuhumiwa na MH. LISSU kupewa fursa ya kusikilizwa na chombo cha kikatiba kilichoundwa kwa mujibu wa IBARA ya 110 ya Katiba;

-haki ya MAJAJI waliotuhumiwa na MH. LISSU kutotendewa kama TAYARI wana makosa anayodai Mh. LISSU mpaka itakapothibitika kwa mujibu wa IBARA ya 110 kuwa wanayo makosa anayodai Mh. Lissu;

Mheshimiwa Lissu hana budi kuheshimu kiapo chake cha kuilinda na kuiheshimu Katiba ya JAMHURI ya Muungano wa Tanzania na afuate utaratibu wa kikatiba badala ya kutumia kinga yake ya Bunge kutuhumu, kuhukumu na kutoa adhabu kwa majaji ambao amewataja kwa majina.

Watanzania ni vyema tukachukua tahadhari dhidi ya watanzania wenzetu ambao wamejiweka katika daraja la juu kuliko hata Katiba na sheria iliyowapa uongozi.

KAMATI ZA MAADILI ZA MAJAJI NA MAHAKIMU

Mwaka jana, Bunge letu lilipitisha Sheria iitwayo JUDICIARY ADMINISTRATION ACT, 2011 (SHERIA YA BUNGE NAMBA 4 YA MWAKA 2011) na MH. LISSU alishiriki kikamilifu katika kutunga Sheria hii inayotoa muongozo wa kupokea malalamiko na tuhuma dhidi ya majaji na mahakimu. Kwa sababu zake mwenyewe, Mh. Lissu ametumia jukwa la kisiasa kulalamika badala ya kufuata utaratibu wa malalamiko ili hao anaodai hawafai waondolewe kwa mujibu wa KATIBA na Sheria.

Kumbu Kumbu za Bunge zinaonyesha ushiriki wa Mh. Lissu kwa ukamilifu. Sheria hii kimeanzisha KAMATI ZA MAADILI ZA MAJAJI, MAHAKIMU NA MAAFISA WENGINE WA SHERIA.
Kwa mfano SHERIA YA BUNGE NAMBA 4 YA MWAKA 2011 imeanzisha Kamati ya Maadili ya Majaji (Judges Ethics Committee) iliyopewa jukumu la:

kupokea tuhuma dhidi ya uvunjifu wa maadili dhidi ya Majaji wa Mahakama ya Rufaa, Jaji Kiongozi na Majaji wa Mahakama Kuu. Tuhuma dhidi ya Majaji hawa ni lazima iwe ni kwa maandishi na iwasilishwe kupitia Katibu wa Tume ya Utumishi wa Mahakama.

Kazi ya Kamati ya Maadili ya Majaji ni kuchunguza Tuhuma na kuwasilisha Maoni yake kwa Tume ya Utumishi wa Mahakama.

Tume ya Utumishi wa Mahakama itasikiliza na kutoa mapendekezo yake kwa Mh. Rais kuhusu kuundwa Tume Maalum ya Kikatiba ya Kumchunguza Jaji.

SHERIA YA BUNGE NAMBA 4 YA 2011 IMEANZISHA KAMATI YA MKOA YA MAADILI

Kila Mkoa unayo Kamati ya Mkoa ya Maadili inayoshughulikia nidhamu ya Mahakimu Wakazi na Mahakimu wa Wilaya (Region, the Regional Judicial Officers Ethics Committee). Kila Wilaya pia inayo Kamati za Maadili ya Wilaya inayoshulikia nidhamu ya Mahakimu wa Mahakama za Mwanzo.

Mh. Lissu anafahamu fika kuwa zipo taratibu za kushughulikia mapungufu au malalamiko dhidi ya Majaji, Mahakimu na Maafisa wengine wa Mahakama. Ila amechagua tu kuwadhalilisha Majaji ili wawe waoga na wasiweze kutoa maamuzi yao bila upendeleo wala uoga.

UKIMYA WA WANASHERIA, WASOMI MAHAKAMA INAPOSHAMBULIWA
Uwoga ni kitu hatari sana katika ujenzi wa demokrasia. Ufundi wa kuongea Bungeni hauna maana kuwa kila kisemwacho na muongeaji mahiri ni sahihi!

Ni kwa bahati mbaya WASOMI, WANASHERIA, magazeti na vyombo vingine vya habari WANA AMINI KUWA KILA KISEMWACHO na Mbunge LISSU ni sahihi na wamefumba macho kuhusu haki ya msingi ya kila mtanzania kusikilizwa na kufuata utaratibu.

MAGAZETI YANAONA KUWA ni sahihi kwa Mh. Lissu kujipa jukumu la kupeleleza “makosa ya majaji”, “kuwatuhumu na kuwatia hatiani majaji” na “kupendekeza adhabu yeye mwenyewe”.

Watanzania tusicheze na haki asilia ya kusikilizwa na umuhimu wa wanasiasa wa wanasheria kuheshimu sheria walizotunga wao wenyewe. Hata MH. LISSU anastahili HAKI asilia ya kutotuhumiwa bila ya kupewa nafasi ya kusikilizwa na kwa utaratibu uliowekwa kisheria.

JE TUHUMA DHIDI YA MAJAJI NI MUENDELEZO WA LENGO LA JAMHURI YETU ISITAWALIKE?
Naogopa kuamini kuwa tuhuma dhidi ya Mhimili wa Mahakama ni muendelezo wa SERA ya kuhakikisha kuwa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania haitawaliki.

Mimi nadhani ni Mhimili wa Mahakama tu ndio ulikuwa umebaki katika mtikisiko huu wa kuhakikisha kuwa Tanzania haitawaliki.
Na njia pekee ni kuwashambulia na kuwashushia majaji heshima mbele ya jamii. Lengo ni kuwafanya Majaji wawe waoga na wasitoe maamuzi magumu.

Kwa Waheshimiwa MAJAJI na MAHAKIMU, huu ni wakati wenu wa kuwa kitu kimoja. Huu ni wakati wa kutokuwa na uoga na kutimiza wajibu wenu kwa mujibu wa katiba, sheria na masharti ya viapo vyenu. JAJI HAONDOLEWI KWA KELELE ZA KISIASA!

Nasikia eti “WANASHERIA-HARAKATI” wametayarisha WARAKA WA KUWAKATAA MAJAJI. WAKILI YEYOTE ambaye anachukuliwa kuwa anaelewa utaratibu wa kuwasilisha malalamiko dhidi ya JAJI au HAKIMU akiwasilisha WARAKA basi huyo WAKILI atakiwe ajieleze kwa nini asitolewe katika orodha ya mawakili kwa kuwa hajui sheria za Tanzania za namna ya kuwasilisha Malalamiko dhidi ya JAJI au HAKIMU.

WANAOTAKA TANZANIA ISITAWALIKE WANAJUA KUWA UKITIKISA MAHAKAMA UNATIKISA UTAWALA WA SHERIA NA UNATIKISA UHAI WA TAIFA LETU.

WANAOTAKA NCHI ISITAWALIKE HUITWA “ANARCHISTS” au “DEMAGOGUES”. Hawa wameongezeka sana chini ya kivuli cha demokrasia na haki ya kusema chochote popote bila kjali sheria yoyote au haki ya mtu mwingine yeyote.

MAHAKAMA MKIYUMBA SISI WANANCHI WA KAWAIDA NDIO TUTABAKI MIKONONI MWA ANARCHISTS na DEMAGOGUES WASIOHESHIMU SHERIA NA AZMA YAO YA TANZANIA ISITAWALIKE itatimia.

MUNGU IBARIKI JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA.