Powered By Blogger

Saturday, July 14, 2012

KESI SASA KUENDESHWA KWA MTANDAO.

Mh. Mathias Chikawe
Waziri wa sharia na Katiba, Mheshimiwa Mathias Chikawe akiwasilisha bungeni mipango na makadirio na matumizi ya fedha ya wizara yake kwa mwaka 2012-2013 amesema serikali kwa Kushirikiana na muhimili wa Mahakama utaanzisha mpango utakaojulikana kama”Tele Justice”, au utaratibu wa kusikutoa kiliza kesi na  haki kwa njia ya Tehama ili kutoa haki hapa nchini na kupunguza gharama kubwa zinazotokana na utaratibu wa sasa.
Mpango huu ambao umezoeleka kwenye nchi zilizoendelea, utaunganishwa magerezani na mahakamani hivyo  utawezesha  kesi kusilikizwa bila ya mtuhumiwa kutolewa gerezani na kupelekwa Mahakamani.

Mh chikawe alisema ya kwamba” utaratibu huu utamuwezesha Jaji au hakimu kusikiliza kesi bila mtuhumiwa kupelekwa Mahakamani, Kwa sasa tunafanya uchambuzi tuanze gereza lipi na Mahakama zipi, ili utekelezaji uanze rasmi kwa mwaka wa fedha 2012-2013”. Mheshimiwa huyo alisema haoni kama itakua shida kwa Mahakama kufanikiwa katika mfumo huo kwani hata Sekta ya mawasiliano hapo zamani ilikua duni sana mpaka kufikia matumizi ya simu za viganjani zinazotumika hivi sasa.

Sanjali na hayo Mh.Chikawe alisema kwamba Mwaka huu wa fedha Serikali inakusudia kuajili Majaji na Mahakimu wa Muda watakaoshughulikia mrundikano wa kesi uliopo hivi sasa. Majaji hao na Mahakimu wataajiriwa kwa Mkataba wa miezi 12 ili kupunguza mashauri takribani (199,741) ambazo bado hazijamalizika.

No comments: