Powered By Blogger

Saturday, July 14, 2012

MAMBO 8 MAZURI KWENYE BAJETI YA WIZARA SHERIA 2012/2013






1.     Serikali iliasaidiana na Mahakama itaanzisha mahakama kuu za wilayani Temeke, Ilala na Kinondoni. Wilaya hizo tatu zitakua kama Mikoa Kimahakama.
2.    Kesi kusikilizwa na kuendeshwa kwa njia ya Mtandao”Tele justice”. Utaratibu huu haumlazimu mshitakiwa au mdaawa wa kesi kufika Mahakamani. Kesi ya Prof.Mahalu ilitumia utaratibu huu.
3.    Serikali ilisaidiana na Mahakama itaajiri Majaji na Mahakimu wa muda” Temporally Judicial Officers”. Kwa kipindi cha miezi 12 ili kupunguza mrundikana mkubwa wa kesi uliopo hivi sasa.
4.    Serikali huenda ikaanzisha Mahakama kuu ya Jinai, itakayokua na mamlaka ya kusikiliza kesi za jinai pekee kama ilivyo hivi sasa kwenye kesi ya kikatiba na kazi.hii itaondoa utaratibu wa hivi sasa wa baadhi ya kesi za jinai kusikilizwa kwenye vikao maalum vya kimahakama katika kesi za jinai(Criminal Court sessions).
5.    Serikali inakusudia kuandaa na kuleta muswada mpya wa sheria ya uhuru wa Habari utakaokua na viwango vya Kimataifa.
6.    Serikali imeanzisha kupitia kwa Ofisi ya Mwanasheria mkuu wa serikali kupita magerezani,kuangalia na kuwaondolea wafungwa walio na kesi zisizo na kichwa wala miguu. Baadhi wa wafungwa wameshanufaika na utaratibu huu.
7.    Mahakama ya Kadhi huenda ikapatikana kwani Serikali bado inamalizia majadiliano na wadau wa Mahakama hiyo. Mahakama hiyo iwapo itaanzishwa iakua na mamalaka ya kusikiliza kesi za mirathi, ndoa na talaka.
8.    Mchakato wa Kupata Katiba mpya huenda ukazaa matunda wakati wa sherehe ya miaka 50 ya Muungano kati ya Tanganyika na Zanzibar hapo tarehe 26.04.2014.

No comments: