Powered By Blogger

Sunday, November 27, 2011

Mh. JAJI SUMARI AZINDUA"SAUT LAW JOURNAL".

 Mh. Jaji sumari akionesha Jarida hilo la sheria

Wadau Mbalimbali waliohudhulio Uzinduzi huo



Mh.Jaji Sumari(Aliyashika Mkasi )akiwa na Sister Hellen mkurugenzi wa Utafiti na uchapishaji wakati wa uzinduzi huo.







Mh. Jaji mfawidhi Aishieli Sumari wa Mahakama Kuu Mwanza, alizindua jarida la sheria" Saint Augustine University Law Journal". linalotolewa na chuo kikuu cha Mtakatifu Sauti jijini Mwanza. Uzinduzi huo ulifanyika siku moja kabla ya Chuo hicho kuadhimisha na kuzalisha wahitimu wa kwanza wa shahada ya  kwanza na ya pili za sheria.

Akielezea umati wa wanazuoni na wanafunzi waliokusanyika katika uzinduzi huo Mh, Sumari alisema kwamba, jarida hilo la sheria lina umuhimu mkubwa sana kwa heshima na hadhi ya chuo husika, kwani ndio kielelezo cha ufanisi wa chuo hicho. Mh. huyo alizidi kusisitiza kwamba nae pia atakua tayari wakati wowote kuandika mambo mbalimbali ya kisheria, kwa manufaa za wasomaji wa jarida hilo.

Aidha, aliwataka waaadhiri wa Chuo hicho katika kitivo cha sheria na waandishi wa jarida hilo kutumia fursa walionayo katika uandishi wa habari mbalimabali za kisheria juu ya mabadiliko yanayoendelea katika jamii yetu hususani  mchakato mzima wa Katiba unaoendelea wakati watanzania wanakaribia kusheherekea miaka 50 ya uhuru. 

Hafla hiyo iliudhuriwa na wanafunzi pamoja na jopo la waadhiri wa chuo hicho na Mapema kabla ya  uzinduzi huo Mkuu wa Chuo hicho Fr. Kitima, Mkuu wa kitivo cha sheria ndugu, Kilangi pamoja na professa Mhalu, walimshukuru kwa nyakati tofauti Mh. sumari kwa kuacha majukumu yake na kuja katika tukio hilo la kihistoria katika Chuo hicho. Walisema Kwamba jarida hio ndilo kielelezo cha ukuaji wa chuo cha Sauti katika kitivo cha sheria.

kwa upande wake Mhadhiri wa chuo hicho, ndugu Innocent Ndanga alionesha kufurahishwa na uamuzi huo wa chuo wa kuchapicha jarida hilo la sheria, na alitoa changamoto kwamba jarida hilo litumike katika kuakisi matatizo mbalimbali ya kisheria yanayowakabili wananchi na jamii kwa ujumla.










1 comment:

Brian Gesase said...

The journal its real very interesting because it contains various essential and contemporary issues which through it, different lawyers have discussed the matters. I think there is a need of having the same in Swahili version as the matter of others' accessibility, who are not able to explore the journal in English.