Powered By Blogger

Thursday, July 28, 2011

Mahakama yamwachia mtuhumiwa wa Richmond.

MAHAKAMA ya Hakimu Mkazi Kisutu imemuachia huru mfanyabiashara Naeem Gire aliyekuwa anakabiliwa na kesi ya kughushi na kutoa taarifa za uongo kuhusu kampuni ya Richmond. Uamuzi huo ulitolewa jana na Hakimu Mkazi Wariyalwande Lema aliyekuwa anasikiliza kesi hiyo. Hakimu Lema alisema upande wa mashtaka umeshindwa kuthibitisha kesi dhidi ya mashtaka waliyomshtaki nayo Gire. 

Alisema ushahidi wa upande wa mashtaka ulikuwa ni dhahifu na kwamba usingeweza kumfanya mshtakiwa huyo ajitetee. “Naiondoa kesi hii chini ya kifungu namba 230 cha Mwenendo wa Makosa ya Jinai kwasababu upande wa mashtaka umeshindwa kuthibitisha mashtaka dhidi ya mshtakiwa,”alisema Hakimu Lema.

 Hakimu Lema alisema hakuna sehemu yoyote ambayo mshtakiwa huyo aligushi na kwamba vitu vyote vilifanywa na Mohamed Gire ambaye ni kaka wa mfanyabiashara huyo.

 Baada ya uamuzi huo, upande wa mashtaka kupitia kwa Wakili wa Serikali, Shadrack Kimaro ulisema utakata rufaa kupinga hukumu hiyo. “Tunaomba tupewe nakala ya mwenendo wa kesi na nakala ya hukumu kwa ajili ya kwenda ngazi za juu zaidi,”alisema Kimaro.Gire alikuwa akidaiwa kuwa, Juni, 2006 jijini Dar es Salaam alitoa taarifa za uongo kwa wajumbe wa timu ya majadiliano ya Serikali, kuwa Kampuni ya Richmond LLC ya Texas, Marekani, ina uwezo wa kuzalisha umeme ili apewe zabuni.

Mfanyabiashara huyo pia alikuwa akidaiwa  kuwasilisha hati ya nguvu ya kisheria iliyotolewa Machi 3, 2006 ikimuonesha kuwa aliruhusiwa na Mwenyekiti wa kampuni hiyo, Hemed Gire ambaye ni kaka yake kufanya kazi za kampuni hiyo hapa nchini.Source Mwananchi

No comments: