Powered By Blogger

Thursday, June 23, 2011

Mh.Jaji aangua kilio akijitetea.

JAJI Atuganile Flora Ngwale wa Mahakama Kuu, Kanda ya Dar es Salaam kitengo cha Ardhi, janaalishindwa kujitetea kuhusu kushindwa kwake kujaza fomu zinazohusu mali na madeni yake, kwa mujibu wa sheria ya maadili ya viongozi wa umma.

Jaji huyo alishindwa kufanya hivyo  mbele ya Baraza la Maadili ambako aliangua kilio na hivyo kusababisha wanasheria kushindwa kumhoji.Hali hiyo ililazimisha baraza kusitisha usikilizaji wa shauri hilo.Wakati akiangua kilio, jaji huyo alilieleza baraza kwamba alishindwa kujaza fomu hizo na kuomba msamaha.Wakati akiangua kilio, jaji huo alisema "sina mali yoyote, kazi ndio maisha yangu, watoto wangu wanategemea kazi hii siwezi kudharau mtu, naomba mnisamehe, nimejifunza Mungu wangu,"alisema jaji huyo.

Jaji Ngwale alisimama katika baraza hilo ili kuanza kujitetea, lakini ghafla aliangua kilio kwa sauti ya juu huku akiomba baraza hilo limuonee huruma kwa kutojaza fomu."Ni kweli sijajaza fomu na kama kuna mtu aliniona nimejaza fomu hizi ajitokeze ndani ya baraza hili la maadili," alisema.

"Kazi hii ndio maisha yangu, kazi hii ndio faraja ya watoto wangu hivyo naitegemea sana  sina mali zozote za kunitesa na kuniita katika Baraza la Maadili,"alisema Ngwale huku akimwaga machozi.


Baada ya Barazakuona Jaji Ngwale ameshindwa kujitetea kwa njia ya mdomo, lilimtaka atoe  utetezi wake kwa njia ya maandishi na kulazimika kusitisha kuendelea na shauri hilo.Mbali na baraza hilo kusitisha kuendelea kusikiliza shauri hilo, pia wanasheria wa sekretarieti ya maadili na hawakupata nafasi ya kumhoji Jaji Ngwale kutoka na hali hiyo.Baada ya baraza hilo kusitisha kuendelea kusikiliza shauri hilo walimuomba jaji huyo aondoke mbele yabaraza hilo, lakini jaji huyo alikaidi agizo la wanasheria hao na badala yake aliendelea kulia mpaka baraza hilo lilipomuomba mmoja wa wanasheria ambembeleze na baada ya kubembelezwa alikubali kwenda kutoa maelezo yake kwa njia ya maandishi na baadaye aliruhusiwa kuondoka.


Baraza hilo litaendelea leo kwa ajili ya kuhoji watu wanne ambao hawakujaza fomu hizo za maadili ya umma mwaka jana, miongoni mwa watu hao watakaohojiwa ni pamoja na Diwani wa Kata ya Kanazi Mathias Bisoma Mgatta, Mkurugenzi wa  Shirika la Hifadhi ya Jamii la Taifa (NSSF), Crecencius  Magori.

Wengine ni Mkurugenzi Mtendaji wa Kikosi cha Usalama Barabarani,  Tafiki Mwanza, Francis Bayona Katunzi na Diwani wa Mpanda mjini Ally Juma Nsokolo.Chanzo gazeti la mwananchi.

No comments: