Powered By Blogger

Wednesday, June 15, 2011

Ashtakiwa kwa jaribio la wizi wa Senti 99(1500 Tsh).

Christopher Tisley

Jamaa hapo pichani ameshitakiwa kwa  jaribio la wizi kwa kutumiwa silaha, Baada ya kumtishia bastola  karani wa duka moja huko Marekani, ili ampe senti 99 za dola ya kimarekani alizokua nazo sawa na shilingi 1500 za kitanzania.

Kulingana na  taarifa  iliyotolewa Mahakama  hapo, Christopher Tisley, 34,  alitembelea maeneo ya Magharibi mwa  Lawrence Avenue huko  Marekani na kumdai karani huyo fedha, karani huyo alipokataa mtuhumiwa huyo alitoa bunduki na kuanza kumtisha nayo.

Tisley,ambae ni mkazi wa Morgan Street, aliamuatoka nje  ya duka hilo baada ya mteja kuingia katika duka hilo, hivyo kumpa mwanya karani huyo kufunga mlango kwa ndani. Japo mlango ulifungwa jamaa huyo aliendelea kugonga malango na madirisha akilazimisha apatiwe pesa. 

Polisi walipofahamishwa walikuja na kukamata  Tisley, japo silaha kwa wakati huo hakua na silaha inayodaiwa alitumia kutishia. Waendesha mashitaka wanasema jamaa huyo alipatikana na gramu 3 ya methamphetamine(unga wenye kemikali) katika milki yake.  

Jaji wa mahakama anayostakiwa jamaa huyo alisema dhamana ya njemba huyo ni Dola 50,0000 sawa na zaidi ya shillingi Millioni 65,000,000/= za kitanzania. Tishley anashitakiwa kwa jaribio la kujipatia mali kwa nguvu na  milki ya mali isiyoruhusiwa.






No comments: