Powered By Blogger

Thursday, April 28, 2011

Fujo Ndani ya ndege zamfikisha rumande.

Bwana Ally Ngenyiki, ambae ni mkazi wa sinza amepandishwa kizimbani katika Mahakama ya wilaya ya Ilala akikabiliwa na mashitaka ya kufanya fujo ndani ya kwenye ndege. wakili wa serikali ndugu, Nassoro katunga alidai mbele ya Hakimu mfawidhi joyce minde kuwa mshitakiwa alitenda kosa hilo tarehe April 23, katika uwanja wa Ndege ya Julius kambarage Nyerere.

Aidha wakili huyo wa serikali alieleza Mahakama hiyo kwamba, mshitakiwa kwa makusudi akiwa ndani ya Ndege alifanya fujo na kuleta usumbufu  kwa muudumu wa ndege hiyo bi. Viviano Shine. Mshtakiwa alikana shitaka linalomkabili, na kurudishwa rumande mpaka mwezi mei, mwaka huu pale kesi itakapotajwa tena.

No comments: