Powered By Blogger

Thursday, August 9, 2012

Malawi Kuishitaki Tanzania Mahakama ya Kimataifa.

Waziri wa MaMambo ya Ndani wa Malawi; Nd.Uladi Musa
 
MALAWI imesema imeondoa ndege zake zilizokuwa zikifanya utafiti wa mafuta katika Ziwa Nyasa kwa kuwa haitaki kuingia vitani, badala yake imeamua kupeleka mgogoro huo Mahakama ya Kimataifa,
Mgogoro baina ya Malawei na Tanzania hivi karibuni uliingia katika hatua nyingine, baada ya Serikali ya Tanzania kuiagiza Malawi kuondosha ndege zilizokua zinafanya utafiti wa mafuta katika eneo lake. Waziri wa Tanzania wa Mambo ya Nje Bernard Membe aliliambia Bunge huko Dodoma  kwamba lazima Malawi iache mipango yake ya kuchunguza mafuta katika ziwa nyasa na kukiita hicho ni  kitendo cha uchokozi.
            
Malawi iliingia mkataba na Kampuni ya Uingereza Surestream mwaka jana kufanya utafiti katika  maeneo ya ziwa  nyasa ambapo  inaaminika kuwa na mafuta na gesi kwa wingi.Hoja ya Tanzania katika mgogoro huu ni kwamba katika sheria za kimataifa  ni kwamba iwapo  nchi mbili zinatengwa  maji, mpaka ni katikati ya  maji hayo na kwamba, Tanzania inapinga umiliki wa Malawi kwa asilimia mia katika ziwa nyasa.

Waziri wa Usalama wa Ndani  wa Malawi Uladi Mussa anasemaje?

Waziri wa Malawi ya Mambo ya Ndani na Usalama wa Ndani, Uladi Mussa, akizungumza na Zodiak Broadcasting Station (ZBS) siku ya Jumanne aliimiza watu katika wilaya mbili za Karonga na Chitipa zinazopakana na Tanzania kubakia shwari kwakua  hakuna kitu ambacho kingetokea.

"Mimi lazima kuwahakikishia watu wote katika nchi hii kubakia shwari. Sisi tuzungumza na serikali ya Tanzania na mambo yote tatakua  mazuri.  Ikishindikana  sisi tutalipeleka suala hilo Mahakama ya Kimataifa ya Haki, " alisema Waziri huyo.Waziri huyo alisisitizakwamba ziwa yote ni ya Malawi na kuongeza kwamba serikali ina ushahidi wa kuthibitisha hatua yake.

"Hakuna suala hapa. Sisi wote tunajua ziwa ni letu. Kwa kweli kama madai kama hayo yangekuja  kutoka Msumbiji angalau ingekuwa inaleta maana  kwa kiasi fulani lakini si Tanzania. Tuna ushahidi wa mikataba kuonesha kwamba Ziwa Nyasa ni mali ya Malawi, "alisema Waziri wa Mambo ya Ndani.

Hoja ya Malawi.

Serikali  ya Malawi inasema kwamba hoja ya  kwa Tanzania-kwamba ziwa litakua la pamoja itatumika pale  tu ambapo hakuna  mkataba lakini katika hali hii mpaka ilikuwa wazi na hasa ilivyoainishwa katika Mkataba wa 1890 Heligoland.

Aidha,  alisema kumbukumbu zinaonyesha kwamba katika 1963 Wakuu wa Nchi wa Shirika la Umoja wa Afrika (OAU) alifanya azimio kwamba nchi wanachama wanapaswa kutambua na kukubali mipaka waliokuwa rithi wakati wa uhuru.

No comments: