Powered By Blogger

Wednesday, August 8, 2012

Hukumu ya Mahalu kutolewa leo.



Prof.Mahalu akiwa na Mawakili wake(Maktaba)

Hakimu Mfawidhi wa Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu Dar es Salaam, Ilvin Mgeta leo anatarajiwa kutoa hukumu ya kesi Na.1/2007 inayomkabili aliyekuwa Balozi wa Tanzania nchini Italia, Profesa Costa Mahalu na aliyekuwa Mkuu wa Fedha na Utawala katika ubalozi huo, bi. Grace Martin, wanaokabiliwa na kesi ya uhujumu uchumi na kuisababishia Serikali hasara.

Hukumu hiyo ambayo awali ilikuwa imepangwa kusomwa tarehe 10 Juali mwaka huu, iliahirishwa na sababu  zikitajwa na Hakimu Aloyce Katemana kuwa ni Hakimu aliyekuwa asome hukumu hiyo, Ilvin Mgeta alipata dharura na hivyo hukumu hiyo ilisogezwa mbele kusubiri atakaporejea.

Kesi hiyo hiyo ambayo imedumu mahakamani hapo kwa miaka saba sasa, ilifunguliwa kwa mara ya kwanza mahakamani hapo Januari 22 mwaka 2007.

No comments: