Powered By Blogger

Thursday, August 16, 2012

DRC: MWANAMUZIKI KOFI OLOMIDE AFUNGWA MIEZI 3.



Koffi Olomide

Mwanzamuziki gwiji wa miondoko ya rumba amefungwa kifungo cha miezi 3 na Mahakama moja ya mjini kinshasa baada ya kukutwa na hatia kwa kuvuruga usalama wa umma. 
 
Mapema jana Koffi alikamatwa kufuatia vurugu katika hoteli moja mjini Kinshasa na kufikishwa mahakamani. Waandishi wa habari wanasema mahakama hiyo ya Kinshasa ilifurika kutokana na watu wengi kuja kumuona kiongozi huyo wa bendi ya Quartier Latin akiwa kizimbani.

Kesi hiyo iliharishwa hadi leo(Alhamisi)asubuhi wakati atakaposhitakiwa rasmi.Wakati wa kesi hiyo hapo jana Koffi Olomide aliwakilishwa na mawakili 10 lakini idadi hio ya mawakili iliongezeka na kufikia 14 .Ugomvi kati ya mwanamuziki huyo na mtayarishi wake Bwana , Diego Lubaki, ni kuhusu pesa dola $3,680.

 Jopo la mawakili wanaomtetea mwanamuziki huyo, huenda ikakata rufaa baada ya kutoridhishwa na kifungo alichohukumiwa mteja wao.

Olomide ni gwiji wa muziki aina ya "soukous", mtindo ulitokana na jina la kifaransa "secouer", lenye maana ya kujitikisa au kujinengua ,na wachezaji wake vile vile wanatambulika kwa kunengua maungo

No comments: