Powered By Blogger

Thursday, July 26, 2012

WAFANYAKAZI GGM WAGOMA: SABABU YA MAFAO YA KUJITOA.

Picha ya Maktaba: Wafanyakazi wakiwa kazini
 
Wafanyakazi wa Mgodi wa dhahabu wa Geita Gold Mine(GGM) wamegoma kufanya kazi sababu kuu ikiwa kupinga sheria  ya mafao ya kujitoa inayowanyiwa wafanyakazi fursa ya kuchukua malipo hayo wanapoacha kazi hadi pale watakapofikisha umri wa kustaafu.  Hali hiyo ilimlazimu Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya uzimamizi na udhibiti wa Sekta ya Hifadhi ya Jamii (SSRA)Bwana Afrikanus Mushi kuzungumza na wafanyakazi hao kwa takriban masaa matatu na kuwaomba warejee kazini, mpaka mamlaka hiyo itakapotoa na kufanya upembuzi yakinifu baada ya mwezi mmoja.
Wafanyakazi kusubiri kama mzee huyu ili wapate mafao
Kauli hii ya Mkurugenzi Huyo wa inakuja baada ya Mamlaka hiyo kupitia katika kitengo chake cha mawasiliano na uhamasishaji kutoa taarifa kwa umma  kwamba “Kufuatia kuanza kutumika kwa Sheria hiyo maombi mapya ya  kujitoa yamesitishwa kwa kipindi cha miezi sita hadi pale miongozo itakapotolewa ili kuiwezesha Mamlaka na Mifuko ya  Hifadhi ya Jamii kutoa elimu kwa wadau”. Haileweki kama kikao hicho cha Mkurugenzi Mkuu na Wafanyakazi wa GGM, kutabadilisha hali hiyo ndani ya kipindi kifupi cha Mwezi mmoja.

Wakati huo huo katika mitandao mbalimbali ya kijamii(facebook, twitter na blogs mbalimbali) wadau wa mitandao hiyo wametoa maoni yao kama ifuatavyo:

Stanslaus Nyambea aliandika: Sheria Kandamizi ya Mafao ya kuacha kazi kabla ya kustaafu yapitishwa Tanzania.Sheria ina mapungufu makubwa ya kisheria:
1. Ina viashiria vya kibaguzi vya waziwazi, yaani mfuko wa hifadhi wa wabunge unasema wanapewa mafao soon after bunge likifa. Kwanini na wao wasiwekewe limit ya miaka 55?-Ubaguzi huu!

Pili, inalazamisha na kuamua matumizi ya mtu binafsi, eti mkopo wa nyumba kwa watu hawa utatolewe na mfuko, wakati hata ukiisha miaka 1000, hutaweza kulipa. Mosi, Kijamii hii sheria ni ya kupuuzi sana; mosi inashau sisi tulioko kwenye sekta binafsi ajira zetu ni za muda.wengi tunajiandaa kwenda kusoma kutumia hizo hela za mafao.

Kisiasa, tunajua kuwa serikali yetu ni mfilisi, haina fedha kwakuwa zinaibwa, hivyo njia pekee ni kuiba fedha zetu za mifuko ya hifadhi kujenga barabara, majengo na kutimiza ahadi za kipuuzi za rai.

Novatus Rukwago aliandika:Hapa kuna maswali machache makubwa ya msingi ya kujiuliza hat kama hatujaanza kutafuta tufanye nini. Hivi hii imepitishwa na nani? 2. Kama ni wabunge tunaowaita wawakilishi wetu, wamefanya hivyo kwa maslahi ya nani?. 3. Je Rais ameshaisain au la. Kama bado, je amesikia kilio cha wnanchi wake? Na kama tayari je alijua alichosain?. Tukipata majibu sahihi ndo tuulizane tufanye maamuzi kwaajili ya leo na kwaajili ya kesho. Mungu atunusuru na msiba huu

Mwingine alisema’ Hiyo Miongozo HATUITAKI.. Mtushirikishe kwenye Miongozo wakati wa KUTUNGA sheria ambayo inatuhusu sisi wenyewe wafanyakazi Hamkutushirikisha why NOW matake kutushirikisha kwenye MIONGOZO? Non Sense kabisa, Hivi wewe mtu amefanya kazi miezi mitatu na kibarua kikaisha na mtu alikuwa analipwa 120,000 Hiyo NSSF yake unajua ni how Much?mpka aisubirie kwa mpk afike miaka 60 na ajira zenyewe hizi za kubangaiza ambazo serikali inaangalia tu wanapewa wageni wazawa tunaachwa unategemea hizi siku zote anaishi vipi? hiyo sheria nafikiri inaweza fanayakazi serikalini ambako watu huwa hawafukuzwi kazi, Kazi inaisha siku anastaafu akiwa na hiyo miaka 60, sisi wa sekta Binafsi Mnatuonea tu, Vimishara venyewe ndo hivyo vya tia maji tia maji, leo hii nimeachishwa kazi nina Miaka 30 ndo ni wait tena 30 years nipewe Hifadhi yangu KWELI? Are you Serious?Please msiwe kama watoto. Hata hii Mamlaka kweli inawatu wenye HEKIMA na BUSARA kweli?Nahisi ni mradi tu wa Mtu, Hiyo mifuko ya jamii yenyewe inapiga Deal kinoma na Hela zetu lakini hatupewi Share kwenye hiyo Miradi wala Riba!Basi wangekuwa hata wanatudanganyishia kutuwekea mdhamana kwenye Mabenki tuwe twapata Mikopo ya Kununua Nyumba za NHC au hata Kupewa Mikopo, As I know kuwa Hii mifuko ya Jamii ina weka Hela zetu kwenye Mabenki kwa FIX deposit accounts..Tunajua yote wanayofanya tuka kaa Kimya NOW ndio mnataka hata hichi kidogo tusikipate,Please Kuweni Serious.


No comments: