Powered By Blogger

Friday, July 13, 2012

MAHAKAMA YAMSAFISHA JOHN TERRY.

John Terry
Terry(31)
 
Nahodha wa zamani wa timu ya soka ya Uingereza Terry(31) , aliyekuwa anakabiliwa na mshataka ya kutoa lugha ya kinaguzi kwa mchezaji mwenzake wa timu ya Taifa ya uingereza hivi punde amesafishwa na Hakimu Mkuu wa Mahakama ya Westiminster, Mh. Howard Riddle kwa kutokupatikana na hatia ya kutoa maneno hayo.

Mwendesha mashtaka katika kesi hiyo alisema kwamba mnamo tarehe 23 Octoba mwaka jana wakati wa mechi ya ligi kuu baina ya CHELSEA  na QPR, Terry alitoa maneno ya kibaguzi kwa mchezaji mwenye asili ya kiafrika Anton Ferdinand.Kesi hii ndio ilipelekea Mcheza soka huyo, Terry kunyanganywa majukumu yake ya unaodha wa timu ya taifa ya uingereza, vilevile ilipelekea kujiuzulu kwa kocha wa timu hiyo Capello. 

Mwendesha Mashitaka katika kesi hiyo bwana Duncan Penny alisema ya kwamba Terry alitoa maneno yafuatayo kabla ya kufungwa mdomo na mchezaji mwenzake wa timu ya chelsea, Obi Mikel; "Fuck off, fuck off", "yeah, yeah", "and", and then "you fucking black cunt, fucking knobhea. 

kesi hii haikua ya kawaida  kwa waendesha mashtaka kwa kua si Anton Ferdinand aliyepeleka malalamiko Mahakamani. polisi walianzisha upelelezi  kama matokeo ya malalamiko yaliyotolewa na afisa moja wa polisi  aliyekua anaagalia mchezo kwenye televisheni. Afisa huyo alisema kwamba Terry alitoa lugha ya kibaguzi kwa mchezaji mwenzake.

Iwapo angepatikana na hatia, Terry angekabiliwa na faini ya Paundi  £ 2,500, takriban shillingi Millioni Tano za Kitanzania.

No comments: