Powered By Blogger

Wednesday, May 23, 2012

Daktari aliyefanikisha kuuawa kwa Osama, ahukumiwa miaka 33 kwa Uhaini.


Dr. Afridi Shakeel
 
Daktari wa Pakistani ambae aliisaidia Marekani kubaini uwepo wa   Osama bin Laden nchini Pakistani amehukumiwa kifungo cha miaka 33 jela      kwa   kosa la       uhaini.

Dokta Afridi Shakeel alishitakiwa kwa kufanya kampeni bandia ya chanjo ya kusaidia CIA kupata sampuli ya DNA ya kiongozi wa al-Qaida na watu wa familia yake ili kuthibitisha uwepo wake katika katika mji huo wa Abbottabad, Pakistan.



Vikosi vya maalum vya Marekani vilimuua bin Laden wakati wa uvamizi uliyofanyika mwaka mwezi wa mei.

Maafisa wa serikali walisema kuwa mahakama ya kikabila iliyopo  kaskazini magharibi ya Pakistan Khyber ilimtia hatia Afridi kwa kosa la  uhaini. Mbali na kutumikia kifungo hicho cha  jela, daktari huyo pia atalazimika kulifaini ya $3,500.Maafisa wanasema kuwa chini ya mfumo wa kikabila, Afridi hakupewa haki ya kujitetea, au kupata mwanasheria.

Mapema mwaka huu, Waziri wa Ulinzi wa Marekani Leon Panetta alisema Afridi alitoa msaada mkubwa sana katika kufuatilia uwepo wa bin Laden  nchini Pakistani hivyo kutoa wito kwa mamlaka ya Pakistan ya kumwachilia. Alisema Afridi angeweza kutoroka Pakistan kabla ya kukamatwa, lakini alichagua kukaa kwa sababu alikuwa na uzalendo.

Alipoulizwa kuhusu hukumu ya  Afridi wa, Msemaji wa Pentagon  George Little aliwaambia waandishi wa habari: " mtu yeyote ambaye amesaidia au kutiamkono Marekani katika kumtafuta Osama bin Laden hastaili kua na kosa kwa kua haikuwa kazi dhidi ya Pakistan bali Walikuwa wakifanya kazi dhidi ya al-Qaida.

Kifo cha Osama bin laden kwa namna moja au nyingine kimefifisha mahusiano ya kidemokrasia kati ya Marekani na Pakistani.

1 comment:

emuthree said...

Mkuki kwa nguruwe, au muosha huoshwa au...?