Powered By Blogger

Wednesday, November 23, 2011

Anusurika kifungo kwa Kumuua Hawara aliyejaribu kumbaka bintiye.


 
Mama lucia Mayunga (umri haukuweza kufahamika mara moja)ameponeakwenda jela baada ya kumuua harawa yake Sadau Elikali  aliyetaka kumbaka binti wa mama huyo.  Mtuhumiwa huyo alipandishwa kizimbani  katika Mahakama kuu kanda ya Mwanza katika kesi no 31 ya Mwaka 2009 na kushtakiwa kwa kosa la kuuwa bila ya kukusidia kinyume cha kifungu cha 195 sura ya 16, kanuni ya adhabu.

Akiongoza upande wa mashtaka  Mahakamani hapo, wakili wa serikali bi, Zaituni mseti aliieleza mahakama hiyo kwamba mtuhumiwa huyo alitenda kosa hilo mnamo tarehe 27.02.2009 majira ya saa nne usiku huko wilayani sengerema.  Alieleza kwamba marehemu na mtuhumiwa walikua na mahusiano ya kimapenzi  kwa muda wa mwezi mmoja kabla ya tukio hilo kutokea, na kwamba siku hiyo majira ya usiku marehemu aliingia nyumbani kwa  Mtuhumiwa bila taarifa ya mama huyo, aliyekua anaishi na watoto wawili wa mdogo wake mmoja wapo akiwa binti wa miaka 15 , kwa jina Magesa Mathias.

Wakili huyo msomi wa serikali, alizidi kueleza Mahakama hapo  , kwamba mara baada ya marehemu kuingia nyumbani kwa mshitakiwa bila ridhaa yake ,alienda  kwenye chumba cha watoto hao waliokua wamelala kisha kuanza kumnyanyua miguu  ya binti huyo mwanafunzi, ndipo binti huyo aliposhtuka na kuanza kupiga kelele. Hali hiyo iliwapelekea watoto hao kukimbia kwa balozi na kutoa taarifa ya tukio hilo.

Ilielezwa na upande wa mashtaka kwamba, baada ya mabinti hao kuondoka, Mtuhumiwa  aliyakua kwenye chumba kingine aliamka baada ya kusilia kelele hizo kisha alichukua fimbo na kuanza kumpiga marehemu  sehemu mbalimbali za mwili kiasi ambacho marehemu alipata majeraha makubwa kichani, yaliyopelekea kifo chake siku moja baadaye.

Akiongoza upande wa utetesi wakili wa Mtuhumiwa ndugu Rutaindurwa aliiomba Mahakama hiyo tukufu  imwachie mama huyo kwani  amekiri mahakamani hapo, na kujutia kutenda kosa hilo, vilevile  marehemu alijitakia kifo chake yeye mwenyewe kwani japokua alikua na mahusiano ya mtuhumiwa bado hakuridhika na kutaka kumbaka binti huyo ambaye ni mtoto wa mdogo wake mtuhumiwa, aliyekua akiishi nyumbani hapo.

Akitoa hukumu hiyo Jaji mfawidhi wa Mahakama Kuu, Mh. Sumari aisema  kwamba kwa kiasi kikubwa marehemu alisababisha kifo chake kwa tendo lake alilotaka kulifanya, pia alihatarisha maisha ya watoto hao waliolazimika kutemba usiku usiku kwenda kwa balozi. Hivyo, kwa busara ya Mahakama mama huyo aliachiliwa huru kwani aliua pasi kukusudia.

No comments: