Powered By Blogger

Tuesday, July 5, 2011

Msaada kizimbani: Nyumba yetu imepata mbia, Tufanyaje??

Habari yako, mimi nilikua nataka kukuuliza suala moja kuhusu mirathi, mimi na family members wenzangu tulikua na mzee wetu ambaye aliingia mkataba na kampuni za ujanja ujanja ili kujengewa nyumba kwa mgao wa asiliamia 30 kwa 70. kwa bahati mbaya Mzee wetu amefariki na sisi baada ya kufungua mirathi tulivyofika kwenye hatua hizo za mirathi ndipo tulipogundua marehemu mzee wetu aliingia kwenye Mkataba huo usiokua na maslahi kwetu. Katika huo Mkataba na masuala yote hayo marehemu mzee wetu hakuwahi kumshirikisha mtoto wake yeyote na pia baada ya Mzee kufariki hatukuwahi kuona karatasi zozote juu ya suala hilo.

Tulipokua kwenye harakati za mirsthi ndipo tulipopewa hati ya ubia baina ya marehemu mzee wetu na kampuni hiyo.Kwamba nyumba yetu ya kawaida itajengwa ghorofa na kwa makubaiano ya asilimia 70 kwa 30.Je sisi tunayohaki ya kuanza nae upya mazungumzo kuhusu mkataba maana bado ipo vile vile huyo mshirika hajaongeza chochote kwenye nyumba mpaka sasa hivi, asante nategemea ushauri wako. Mr.B

No comments: