Powered By Blogger

Wednesday, July 6, 2011

Breaking newzzz......Hali ya hewa yachafuka mwanza!Risasi za moto zatumika.


Hali ya jiji la mwanza leo hii imechafuka baada ya polisi kupambana na machinga waliotakiwa kutolewa katika maeneo kadha wa kadha katikati ya jiji. Habari zilizoifikia blog hii ni kwamba takriban watu watatu wameuawa katika sakata hilo, maduka kuvamiwa na vibaya na mali kuporwa ikiwemo magari yaliyo katika maeneo ya karibu kuharibiwa vibaya.
Jamaa akijiandaa kurusha jiwe

Umati katikati ya hekaheka

Vibanda vimevunjwa, Baadhi ya bidhaa zilizopangwa nje zimeibiwa nayo matairi yamechomwa katikati ya njia panda kuingia mtaa wa Makoroboi kuelekea Soko kuu na kiunganishi cha barabara ya Lumumba Mwanza huku baadhi ya wamachinga hao wakirusha maboksi yaliyoshika moto kwenye majengo yaliyo karibu na eneo hilo.kamanda wa Polisi hakuweza kupatikana kuelezea vurumai izo.



No comments: