Powered By Blogger

Thursday, June 16, 2011

Mtikila Kuishitaki Serikali Mahakama ya Afrika:Adai Mabilioni.

Mchungaji Christopher Mtikila,

MWENYEKITI wa Chama Cha DP, Mchungaji Christopher Mtikila, ametangaza kesi mpya nne za kimataifa dhidi ya serikali ikiwemo madai ya fidia ya dola zamarekani milioni 150.Akizungumza na waandishi wa habari Dar es Salama jana, Mchungaji Mtikila alisema amefungua kesi katika Mahakama ya Afrika ya Haki za Binadamu na kwamba tayari aliziwasilisha Juni 10 mwaka huu na itaanza kusikilizwa muda wowote kuanzia sasa.

Alisema kesi hizo nne dhidi ya serikali pia ina kipengele alichodai kuwa ni kubatilishwa kwa uhuru wa Tanganyika na muungano pamoja na baadhi ya vipengele vya katiba.Alitaja vifungu vya katiba anavyopinga kuwa ni ibara ya 39, 67 na 77, kufungwa jela mwaka mmoja kwa kile 'bila kosa' na madai ya mke wake, Bi. Georgina Mtikila kudhulumiwa mamilioni ya fedha.

Alisema katika kesi hizo anatetewa na jopo la wanasheria waandamizi sita wa kimataifa ambao walikuwa wa Umoja wa Mataifa (UN).Aliwataja wanasheria hao wanaosimamia kesi zake kuwa ni Profesa. Setondji wa shirika la Etudes Vihode la Benini, Prof. Charles Adeogun wa shirika la Charles Antony LLP (Nigeria), Profesa Frscis Dako wa Benini wakisaidiwa na Bi. Mary Birdi, Profesa Deogratias Njau na Prof. Megan Thompson wote wa Benini.

Mchungaji Mtikila alidai kuwa kitendo cha uhuru wa Tanganyika kubatilishwa na kuungana na Wazanzibari hakikubaliki na kwamba kinakwenda kinyume cha matakwa ya wananchi.Alisema uhuru huo ndio haki kuu ya watu wote duniani ambao ilisababisha kuundwa kwa Umoja wa Mataifa mwaka 1945 (The right to self Determination).

Alisema uhuru wa Watanganyika ni haki ya Watanganyika wenyewe hivyo wana wajibu wa kuutunza uhai wao katika mipaka ya ardhi kwa utaratibu wao wenyewe kwa kutumia maziwa na asili yao.Alidai kuwa Baba wa Taifa hayati Julius Nyerere, anastahili kuhukumiwa hata kama ni marehemu kwa kuhusika katika kuwapunguzia Watanganyika ubinadamu na kulazimishwa kuwa 'watumwa wa Wazanzibari'.

Mchungaji Mtikila alitoa mpya pale alipodai kuwa katika orodha ya watuhumiwa hao, Hayati Nyerere yumo na atahukumiwa kama akipatikana na hatia kwa sababu alilazimisha watu kuwa 'watumwa wa nchi nyingine jirani' na kupunguza umuhimu wao na hatimaye kupoteza kabisa utambulisho wa nchi yao Tanganyika.

"Tunataka mahakama ya kimataifa itupatie haki ya uhuru wetu (The right to self determination of the people of the Republic of Tanganyika) kama binadamu wengine wote katika mipaka ya nchi zao, tunaiambia mahakama ya ulimwengu kwamba muungano ni kongwa la utumwa katika chingo la Tanganyika," alisema.

Kuhusu kufungwa mwaka mmoja jela alisema kuwa alifungwa kwa sababu ya kukemea na kukaripia kuhusu alichokiona juu ya kifo cha aliyekuwa Katibu Mkuu wa CCM, Marehemu Horace Kolimba ambapo mahakama ya rufani ilimuhuku kutokana na kauli alizozitoa kama kiongozi wa dini.

Alidai amefungua kesi upya katika mahakama hiyo akitaka serikali kumlipa dola milioni 150 za kumfunga na kumdhalilisha bila kosa.

Alisema madai ya mke wake alifikishwa mahakamani mwaka 1984 na kuendeshwa kisiasa na hatimaye kutolewa hukumu mwaka 1994 kwa kuyatupilia mbali. Habari hii chanzo chake ni gazeti la Majira.

1 comment:

Anonymous said...

I think Mtikila maybe right and has a cause of Action not only agaist the Late Mwl. Nyerere but also against Mkapa who disregarded Majority opnion collected by R.Kisanga-J Commission. In his report learned brother Kisanga was clear and open that the majority of Tanzanians were claiming to resume to their Tanganyika as their Nation, which susquently would form the United Republic of Tanzania without loosing its identity. I stand to be corrected
su