Powered By Blogger

Monday, June 27, 2011

Hati ya kumkamata Gadaffi yatolewa.

Kanali Mohamed Gaddafi

Mahakama ya kimataifa ya uhalifu wa kivita imetoa hati ya kukamatwa kwa kiongozi wa Libya Kanali Muammar Gaddafi.Mahakama imemtuhumu kwa uhalifu dhidi ya binadamu na kuamuru mashambulio kwa raia baada ya machafuko dhidi yake kuanza kati kati ya mwezi Februari.

Mahakama hiyo iliyopo the Hague pia imetoa hati ya kukamatwa kwa washirika wake wakuu Kanali Gaddafi- mtoto wake wa kiume Saif al-Islam na mkuu wa kijasusi Abdullah al-Sanussi. Maelfu ya watu wanaaminiwa kufariki dunia kwenye ghasia hizo.

Hati hizo ziliombwa na mkuu wa mahakama hiyo ya ICC Luis Moreno-Ocampo mwezi Mei, aliyesema watu hao watatu walihusika na "mashambulio yaliyopangwa na yaliyosambaa" kwa raia.Bw Moreno-Ocampo alisema mahakama hiyo ina ushahidi kuwa Kanali Gaddafi "aliamuru binafsi mashambulio kwa raia wa Libya wasio na silaha na alihusika kwa kukamatwa na kunyanyaswa kwa wapinzani wake wa kisiasa.

Serikali ya Libya hivi karibuni ilisema haitambui mahakama hiyo na tishio la hati hiyo haiwashughulishi.

No comments: