Powered By Blogger

Sunday, July 8, 2012

MAWAKILI NA WAZEE WA BARAZA KATIKA MAHAKAMA ZA MWANZO.



 1.0 UTANGULIZI


Kwa miongo mingi sana, Mashauri mbalimbali katika Mahakama za Mwanzo yamekua yanaongozwa na Mahakimu wasio wanasheria pamoja na wazee wa Baraza. Mawakili kama maofisa wa Mahakama hawakupewa na nafasi kuwawakilisha wadaawa mbalimbali katika Mahakama hizo za Mwanzo.  Kimsingi Waraka wa maendeleo ya UTUMISHI WA Umma Namba 1 wa mwaka 2010, umeondoa au kufuta nafasi za Mahakimu wa Mahakama za Mwanzo na kuwaweka Mahakimu wakazi wa Mahakama za Mwanzo.

Mabadiliko haya kwa namna moja au nyingine yatapelekea kuwepo mabadiliko ya sheria , na pengine kuakisi nafasi na umuhimu wa Mawakili na Wazee wa Baraza katika Mahakama za Mwanzo nchini.

1.0   NAFASI NA UMUHIMU WA MAWAKILI KATIKA MAHAKAMA ZA MWANZO
Baadhi ya Mawakili wapya walioapishwa Juzi


Ibara ya 13(6)a ya Katiba ya Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania, 1977 inaeleza ya Kwamba kila mtu ana haki ya kusikilizwa, Haki ya kusikiliza kwa namna moja au nyingine huusisha haki ya kuwakilishwa na Mawakili katika Mahakama za Mwanzo. Kimsingi wananchi wengi wamekua wakiikosa haki hii muhimu, iliyowekwa kikatiba pia kutolewa Maamuzi mbalimbali kama mojawapo ya msingi wa “principles of natural justice”.  Wananchi wamekua wakiikosa haki hii kutokana na mfumo na muundo wa Sheria zilizopo zinazowanyima Mawakili nafasi za kuwawakilisha wateja wao katika Mahakama hizo za Mwanzo kama ilivyobainishwa katika  Sheria ya Mahakama Sura ya 11, Rejeo la Mwaka 2002.

Kuna na umuhimu mkubwa iwapo mawakili watapewa nafasi kisheria kuwawakilisha wateja wao katika Mahakama za Mwanzo kama ifuatavyo;

a. Kupunguza mrundikano wa kesi Mahakamani, mawakili Kama maofisa wana majukumu ya kisheria kuisaidia Mahakama kutoa Maamuzi ya Haki. Iwapo pande za wadaawa zitawakilisha na Mawakili Mahakamani, yumkini mashauri mengi yatamalizika mapema, hivyo kuondoa Mrundikano wa kesi usio na tija Mahakamani.

b. Kumalizika Kwa Mashauri kwa Wakati, iwapo Mawakili watapata fursaya kuwawakilisha wateja wao katika Mahakama za Mwanzo. Watawaongoza wadaawa au wateja wao kutatua migogoro yao kwa kutumia njia mbadala za kutatua migogoro hiyo yaani” Alternative Dispute Resolution”.

c. Wadaawa kupata haki yao ya kuwakilishwa, kama ilivyobainishwa hapo awali sio kila mtu ana uwezo wa kusimama mbele ya Mahakama ya kujitetea. Iwapo Mawakili watapata fursa ya  kuwawalisha wateja wao hii itatoa fursa kwa wadaawa wao kupata  ya kuwakilishwa ipasavyo katika mashauri yanawayowakabili.

d. Ajira, Kuanzishwa kwa Shule ya Sheria Nchini” Law School of Tanzania”, kwa namna ya pekee kumepelekea ongezeko kubwa la Mawakili nchini, wengi wa mawakili hao ni Vijana wasio na fursa ya kuajiliwa Serikalini, au Taasisi mbalimbali kutokana na ufinyu wa ajira Nchini. Hivyo basi nafasi hii itatua fursa ya ajira kwa Mawakili wengi kuwawakilisha wateja wao hasa kwa wananchi wengi walio vijijini ambapo kuna Mahakama Nyingi za Mwanzo.

2.0   NAFASI NA UMUHIMU WA WAZEE WA BARAZA KATIKA MAHAKAMA ZA MWANZO.

wazee wa Baraza wamekua Wakitumika si katika Mahakama za Mwanzo pekee Vilevile Katika  Mahakama Kuu, Wazee hawa wamekua na Mchango mkubwa sana katika kuisadia Mahakama Kutoa maamuzi ya haki.  Kifungu Cha 7(1) Cha  Sheria ya Mahakama, Sura ya 11 ya Mwaka rejeo la Mwaka 2002, Kinatoa akidi ya Mahakama katika mwenendo wa Mashauri katika Mahakama za Mwanzo ya Kwamba panatakiwa katika kila shauri pawepo na wazee wa baraza wasiopungua wawili.
Na kwamba, maoni ya wazee wa katika Mahakama za Mwanzo ni ya Muhimu na lazima yazingatiwe katika utaoaji wa maamuzi ya haki.  Na kwamba Mahakimu ni lazima wazingatie maoni ya Wazee hao wa baraza.
Swali la kujiuliza ni kama iwapo Mawakili wataruhusiwa kuwawakilisha wateja wao katika Mahakama za Mwanzo Je kuna ulazima wa wazee wa Baraza kuendelea kuwepo?

Ni rai yangu kwamba wazee wa Baraza Bado wanaumuhimu Mkubwa sana kuendelea kuwepo( kama nitakavyoelezea hapo baadae wapepo katika misingi gani). Kwa uchache umuhimu wa Wazee wa Baraza ni kama Ufuatao;

a. Kwa kua Mahakama nyingi za Mwanzo zipo vijijini, ambapo kuna kesi nyingi sana za zinazohusisha mambo ya Kimila. Wazee wa Baraza ni muhimu hasa katika kuisadia Mahakama Kupata tafsiri mbalimbali za Kimila hasa katika masuala ya Mirathi, Ndoa  na…Kwa Mfano katika jamii ya kisukuma kuna faini ya “ Misango na Ngweke” (hii ni faini ambayo anapewa kijana kwa ajili ya utorosha binti). Uwepo wa wazee hawa kutasaidia sana Mahakimu wa Mwanzo Wakazi katika masuala ya kimila ya Ndoa, Mirathi na madai.
3.0   MUUNDO WA MAHAKAMA
Kwakua Mahakama za wilaya na Hakimu Mkazi zina nguvu sawa katika usikilizaji wa Mashauri ya mbalimbali hususan ya madai. Ni rai yangu kwamba hakuna haja ya kuendelea kua na Mahakama 2 tofauti. Mahakama hizi zingeunganishwa na kupatikana na Moja. Kwani kwa kawaida Rufani za , Mahakama hizi huenda Mahakama Kuu. Kwa mantiki hii basi Muundo huu wa Mahakama shurti ubadilishwe.

4.0   MAPENDEKEZO (NINI KIFANYIKE)
Ni ukweli usiopingika Kwamba Mawakili na uwepo wa Wazee wa Baraza katika Mahakama za Mwanzo nchini una maana kubwa katika kuziboresha Mahakama zetu, ili kutoa maamuzi ya haki na kwa wakati. Ili kufanukisha yote haya yafuatayo yanapaswa kuzingatia na kufanyika;
a.  Madadiliko ya Sheria, Vifungu mbalimbali vya kisheria ni lazimavibadilike katika mantiki ya kuwawezesha Mawakili kuhudhuria Mashauri ya Mahakama za Mwanzo kama ifuatavyo;
          i.     Kifungu cha 33(1) kinachowazuia Mawakili kutowawakilisha wateja wao katika Mahakama za Mwanzo kirekebishwe kutoa Mwanya kwa Mawakili hao kua na fursa hiyo.
        ii.     Kifungu cha 7(1) Cha Sheria Ya Mahakama, Sura ya 11,Rjeo la Mwaka 2002 kinachosema; in every proceeding in Primary Court, including a finding, the Court shall not sit with not less than two assessors.

Ni rai yangu kwamba kwa majukumu ya wazee wa baraza yawe kwenye kesi za madai pekee wa wasipewe nafasi katika kesi ya Jinai kama ambayo Kifungi tajwa hapo juu kinavyobainisha” in ever proceeding” mabadiliko yafanyike ili kuwe na ukomo kwenye mashauri ya jinai yaani” in Civil proceedings in Primary…..” Hii ni kwakua wazee hawa hawana weredi wa makosa mbalimbali ya kisheria.
b. Maoni ya wazee wa Baraza, kwa hali ilivyo hivi sasa maamuzi ya Mahakama ya Mwanzo yanategemea maoni ya Wazee Wa Baraza. Sheria ibadilishwe ili maoni haya ya wazee wa Baraza yewe” not binding” ili kulinda na kuakisi dhana nzima ya uhuru wa Mahakama” Independence of Judiciary”.
c. Miundombinu ya Mahakama za Mwanzo; Mahakama nyingi za Mwanzo zipo vijijini vikiwa na Miundo mbinu mibovu sana, majengo yaliyochakaa hivyo haitokua busara kwa Mahakimu Wakazi tarajiwa wa Mahakama hizo kufanya kazi katika Mazingira haya. Ni rai yangu kwamba za juhudi za hali na mali zifanyike kuboresha mazingira haya ya Mahakama hizi.
d. Lugha ya Mahakama; Kwa hali ilivyo hivi sasa Mashauri ya Mahakama ya Mwanzo yanaendeshwa kwa lugha ya Kiswahili. Iwapo Mawakili wataruhusiwa kuingia katika Mahakama hizi basi Lugha ya kiingereza itumike kama Mbadala wa Lugha ya Kiswahili. Hivyo basi kifungu cha 13(1) Cha Sheria ya Mahakama, Sura ya 11 rejeo la mwaka 2002 kinachosemeka “the language of primary Court shall be in Kiswahili”.
5.0   HITIMISHO
Ni Rai yangu kwamba nafasi ya Mawakili katika utoaji wa maamuzi ni mkubwa sana, Sheria Zetu zibadilishwe ili kuakisi hali halisi ya mabadiliko haya.

No comments: