Powered By Blogger

Thursday, December 1, 2011

JAJI MKUU ASHINDWA KUMRITHI OCAMPO ICC

Bi Fatou Bensouda

BI.Fatou Bensouda pichani kutoka Gambia imeibuka kidedea  akatika mchakato wa maridhiano wa kumtafuta  mwendesha mashtaka mkuu wa Mahakama ya Kimataifa ya Jinai.Bensouda mwenye umri wa miaka 50, ni naibu wa mwendesha mashitaka mkuu wa sasa, Luis Moreno-Ocampo wa Argentina, ambaye muda wake unamalizika  mwaka ujao.Mkutano wa wanachama wa ICC utafanyika mjini New York  Alhamisi  wiki ijayo kujadili uteuzi.


Bensouda amekua  mwendesha mashitaka msaidizi wa ICC Hague toka mwaka 2004 na awali alifanya kazi kama mshauri wa kisheria na wakili wa kesi katika Mahakama ya Kimataifa ya Mauaji ya Kimbari ya Rwanda mjini Arusha, Tanzania.Yeye kwa muda mrefu amekua akionekama kama mtu atakayechukua nafasi za Moreno-Ocampo, hasa wakati ambapo kesi za ICC kwa kiasi kikubwa zimelenga Afrika.

Bensouda alikuwa mmoja wa wagombea waliotajwa na kamati ya kutafuta mrithi wa Ocampo  mwezi uliopita kuchukua nafasi Moreno-Ocampo kama mwendesha mashitaka mkuu wa mahakama ya duniani juu ya uhalifu wa kivita;wengine walikuwa wa mwiingereza Andrew Cayley,  Mohamed Chande Othman, Jaji Mkuu wa Tanzania, na Robert Petit, mshauri ya uhalifu wa kivita katika Idara ya Haki nchini Canada.

Mwanadiplomasia mmoja wa umoja wa Mataifa  ambaye hakutaka kutambuliwa aliliambia shirika la habari la Reuters kwamba Jaji Mkuu wa Tanzania Othman alijitoa katika kinyanganyilo hicho.

 
Katika maendeleo ya hivi karibuni kuwashirikisha ICC, rais wa zamani wa Ivory Coast Laurent Gbagbo alipelekwa the Hague  Jumanne usiku kukabiliana na mashtaka ya uhalifu dhidi ya binadamu yanayomkabili.


Baadhi ya wanasiasa wa Afrika wanamshutumu  mshitakiwa Moreno-Ocampokwa kutafuta na kuwashitaki Waafrika tu.
Ocampo pia imekosolewa juu ya maendeleo ya ICC polepole na kwa kushindwa kuleta idadi kubwa ya viongozi waandamizi wa serikali kwa ajili ya kesi ya mauaji mbalimbali.

1 comment:

Profee said...

Nimependa sana fonts, contents arrangement ya hii blog bt tupe wadau wako Updates zaidi.
Ukiweza pitia
www.TanzaniaKwetu.com
na if possible jaribu kuisajili blog yako kule jus kuongeza viewers.

Tupo pamoja Mtanzania!