Powered By Blogger

Thursday, July 14, 2011

Anusuriki kifungo kwa kumuua mumewe kwa kipigo

Mshtakiwa Letisia Kasabuka amenusurika kwenda jela kwa kumuua mumewe bila ya kukusudia kinyume na  kifungu cha 195 na 198 Cha sheria ya makosa ya Jinai Sura ya 16 kama ilivyofanyiwa marekebisho mwaka 2002.

Akiieleza Mahakama wakili wa Serikali Ndugu Kamala, alisema kwamba mnamo  tarehe 28.12.2008 majira ya usiku mtuhumiwa na marehemu mumewe walikua nyumbani kwao huko Geita. Wakiwa nyumbani hapo ugomvi ulizuka baina yao ivyo kupelekea kuumizana.

Wakili huyo, aliendelea kukiambia Kikao hicho cha Mahakama Kuu kanda ya Mwanza kwamba hali ya mume wa mshtakiwa ilidhoofu kesho yake kutokana na kipigo kilichotolewa na mama huyo hali iliyolazimu kupelekwa Hospitalini, kabla ya kuhamishwa kwa mganga wa kienyeji.

Mshtakiwa alikiri mbele ya Mh.Jaji G.K.Mwakipesile hivyo wakili wake wa utetezi, kuiomba mahakama hiyo tukufu imuonee huruma mtuhumiwa huyo kwani ni mama wa watoto wanne na alifanya kosa hilo bila ya kukusudia pia ana motto mdogo aliyemuacha na mwaka mmoja . Kwa upande wake ndugu kamala aliiomba Mahakama  itoe adhabu kali ili iwe fundisho kwa akina mama wenye tabia ya kupiga waume zao.


Hata hivyo Mh.Jaji G.K Mwakipesile aliamuru mtuhumiwa kuachiwa huru, kwa kuua bila ya kukusudia. Chini ya kifungu cha 326(1)b cha Sheria ya mwenendo wa Mashtaka Sura ya 20, kama ilivyofanyiwa marekebisho mwaka 2002.

No comments: