Powered By Blogger

Wednesday, June 29, 2011

Afungwa kumuua rafikiyake: Kisa kaambiwa alipe bili ya bia.


Mshtakiwa Juma Mwita ameshtakiwa na kuhukumiwa na Mahakama kuu kanda ya Mwanza katika shitaka la jinai No. 10 la mwaka 2007 kwa kosa la kusababisha bila kukusudia mauaji ya rafikiye kalyankozie mujuni kinyume na kifungu cha 195 cha Sheria ya makosa ya jinai, ya mwaka 2002. Karani wa mahakama Kuu bi Shida liieleza mahakama hiyo tukio hilo lilitokea huko katika visiwa vya maisome Sengerema.

Akiiieleza mahakama hiyo wakili msomi wa serikali Ndugu; Obadia alisema kwamba mnamo tarehe 22/06/2007 mshtakiwa akiwa na rafiki zake walikua wanakunywa katika baa ya marehemu (kalyankozile mujini).

Baada ya kunywa kwao, rafiki wa mshtakiwa ndugu kalyankozile ambae pia alikua mmiliki wa grocery aliamua  kumuandikia Mtuhumiwa bili ya bia zote alizokunywa marehemu ili mshitakiwa azilipe. Mshtakiwa alikataa kulipa ndio mzozo ulipozuka baina yao. Mshtakiwa aliamua kumsukuma marehemu hivyo kumsababishia maumivu makali.

Aidha wakili huyo wa serikali aliiambia mahakama kwamba siku moja baadaye, marehemu kutokana na maumivu hayo alishindwa kwenda kazini hali hiyo iliendelea  mpaka tarehe 1/7/2007 mauti ilipomfika.


Mshtakiwa alikiri kosa lake hivyo kumlazimu Mh.Jaji G.K. Mwakipesile kumtia hatiani na kumfunga kifungo cha miaka 5 nje kwa mujibu wa kifungu cha 326(1) cha Sheria ya mwenendo wa Mashtaka kama ilivyofanyiwa marekemisho Mwaka 2002; ili iwe fundisho kwa watu wengine.

No comments: